Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Senegal: AU yatoa wito wa kufanyika mazungumzo

Rais Wa Senegal Aahirisha Uchaguzi Senegal: AU yatoa wito wa kufanyika mazungumzo

Mon, 5 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat, ametoa wito wa kusuluhishwa kwa mizozo ya kisiasa nchini Senegal kupitia njia ya mazungumzo na mashauriano.

Wito wa AU umekuja baada ya kushuhudiwa makabiliano kufuatia hatua ya kuhairishwa kwa tarehe ya uchaguzi mkuu wa mwezi huu.

Faki aidha ametoa wito kwa mamlaka kuandaa uchaguzi huo haraka kama ilivyopangwa na kwa njia ya uwazi na haki

Rais wa Senegal Macky Sall alitangaza kuwa uchaguzi wa tarehe 25 ya mwezi Februari umehairishwa.

Wito wa AU unakuja wakati huu pia wabunge nchini humo wakitarajiwa pia kukutana kujadili hatua hiyo ya Sall ambayo imeibua mzozo kwenye taifa hilo.

Wabunge hao wanakutana siku moja baada ya kutokea kwa maandamano jijini Dakar, tukio ambalo lilipelekea kukamatwa kwa mwanasiasa wa upinzani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live