Wed, 17 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Rwanda, limethibitisha kumuua mwanajeshi mmoja wa DRC na kuwakamata wengine wawili, baada ya kuvuka mpaka wao na kuingia nchini humo kwenye mpaka wa wilaya ya Rubavu usiku wa kuamkia leo.
Wanajeshi hao wanadaiwa kuingia nchini Rwanda kupitia mpaka wa Rubavu.
Jeshi la Rwanda kupitia ukurasa wake wa kijamii wa X, limesema mwanajeshi huyo aliuawa wakati alipojaribu kuwafyatulia risasi askari wake waliokuwa doria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live