Tue, 30 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Naibu Rais William Ruto amefika katika majengo ya bunge tayari kuhudhuria mkutano wa Rais Uhuru Kenyatta ambapo anatarajiwa kuhutubia taifa.
Ruto ambaye amekuwa akisusia baadhi ya mikutano ya kitaifa alikaribishwa na maafisa wa kijeshi na maspika wa mabunge mawili majira ya saa nane na thelathini na tisa.
Rais anatarajiwa kuhutubia bunge la kitaifa pamoja na la seneta na pia kuangazia mafanikio yake kwa kipindi cha miaka 8 ambayo amekuwa madarakani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live