Rais wa Jamhuri ya Kenya ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Kenya Dkt. William Rutto amemteua na kumuapisha Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Wanamaji na Naibu Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Kenya (VCDF) kuwa Mkuu wa Majeshi mpya wa Majeshi ya ulinzi na usalama (CDF) nchini humo, akichukua nafasi ya Jenerali Francis Omondi Ogolla aliyefariki kwa ajali ya helikopta Aprili 18.2024
Rais wa Jamhuri ya Kenya ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Kenya Dkt. William Rutto amemteua na kumuapisha Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Wanamaji na Naibu Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Kenya (VCDF) kuwa Mkuu wa Majeshi mpya wa Majeshi ya ulinzi na usalama (CDF) nchini humo, akichukua nafasi ya Jenerali Francis Omondi Ogolla aliyefariki kwa ajali ya helikopta Aprili 18.2024 Luteni Jenerali Kahariri ambaye pia amepandishwa cheo kuwa Jenerali Aprili 18.2024, sasa ana wajibu wa kuongoza maziko ya Jenerali Francis Omondi Ogolla kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Kenya nafasi ya CDF haipaswi kuwa wazi lakini pia CDF huzikwa na CDF mwenzake.