Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto asema umaarufu wake ulitokana na Rais Kenyatta

0fgjhs1uml0dm7udo Ruto asema umaarufu wake ulitokana na Rais Kenyatta

Tue, 26 Oct 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

William Ruto amedai kwamba Rais Uhuru Kenyatta alimpa baraka za kuwania kiti cha kumrithi kisiasa.

Ruto amesema kwamba Uhuru alimwambia awatembelee wenyeji wa Mt Kenya katika makanisa na kuwpa ahadi kwamba watajengewa barabara na shule ili kuiteka mioyo yao Walakini, Uhuru, ambaye wengi wametabiri kwamba atamuunga mkono kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga, amekuwa akimkashifu vikali naibu wake kwa kuanza mapema kampeni za 2022.

Naibu Rais William Ruto amedai kwamba Rais Uhuru Kenyatta alishampa baraka za kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa 2022.

Baraka za Uhuru

Kulingana na Ruto, mkubwa wake alimshauri jinsi anavyopaswa kufanya kampeni zake ili kuteka nyoyo za wapiga kura.

Ruto alisema umaarufu wake katika eneo la Mt Kenya ulifanikishwa na mawaidha aliyopewa na Uhuru.

“Nina baraka kutoka kwa rais, tayari alinishauri jinsi ninavyopaswa kupiga kampeni, ndio maana sing'anga'ni sana," Ruto alisema.

Huku akiwahutubia waumini wa kanisa la Later Glory Worship Center eneo la Gachie, Kaunti ya Kiambu mnamo Jumapili Oktoba 24, Ruto alisema kwamba Uhuru alimshauri awe anayetambelea makanisa.

"Aliniambia niteke nyoyo za wenyeji na nianze kuukwea mlima bila wasiwasi. Pia aliniambia ninafaa kuyatembelea makanisa na kuwapa ahadi za kujenga barabara na kuboresha elimu miongoni mwa mambo mengine," Ruto alisema.

Ruto alipoteza mwelekeo Hata hivyo tamko la Ruro lilikinzana na la rais ambaye alimkashifu vikali kwa kuanza kampeni za mapema za uchaguzi mkuu wa 2022. Uhuru alimuambia Ruto kutuliza boli katika azma yake ya kuwania urais "kwa sababu muda haukuwa umewadia".

“Mimi na ndugu yangu Ruto, tulikuwa tukitembea pamoja hadi 2022 ilipoingia kwenye mpango. Alipoteza mwelekeo. Ningependa kumwambia awachane na siasa za 2022. Hiyo itakuja. Wacha awe na subira.”

Uhuru aliyasema haya wakati alipokuwa akizindua rasmi ripoti ya BBI katika ukumbi wa Bomas of Kenya mwaka wa 2020.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live