Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto asema ni kosa kwa Gavana kumpokea Raila

657899546b1f9b2c Ruto asema ni kosa kwa Gavana kumpokea Raila

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Alisema Raila hana rekodi ya kuchapa kazi kwa wakazi wa Kiambu na hivyo hafai kufanyiwa kampeni hukoAlimtaka Nyoro kukoma kumkaribisha Raila katika kaunti hiyo akisema wakazi watanufaika ndani ya UDAWakati wa ziara hiyo Ruto alipata mfuasi mpya baada ya aliyekuwa mbunge wa Thika Alice Ng'ang'a kujiunga na UDANaibu Rais William Ruto alimtupia mishale ya kisiasa Gavana wa Kiambu James Nyoro akisema anashirikiana na viongozi wazembe.

Ruto alikosoa Nyoro kwa kumkaribisha Raila Kiambu akidai kuwa kiongozi huyo wa upinzani hana mpango wowote kwa wakazi.

Alisema hatakubali baadhi ya viongozi kwenye muungano wa Jubilee kuwauzia wafuasi wa Mt Kenya Raila kama mgombea wa urais.

"Tumeunda serikali mara mbili. Yaani hatuwezi kumuunga mmoja wetu kuongoza mpaka sasa tumeenda kwa ule mtu wa kitendawili? Apana hilo haliwezekani, hiyo ni matusi na madharau," alisema Ruto alipozuru kaunti hiyo Jumamosi Novemba 13.

Alipigia upato serikali ya UDA akisema ndiyo itabadili maisha ya Wakenya na kumtaka Nyoro kutowapeleka wakazi kambi ya Raila.

Read also

"Ulinyaganywa Bibi Juzi": Ichung'wah Amrushia Gavana Mutua Vijembe

"Raila hana rekodi ya kuchapa kazi. Nataka nimwambie Gavana wa Kiambu James Nyoro kuwa tuna akili, amekuwa akileta Raila hapa na anajua Raila hana rekodi ya kuchapa kazi," Ruto alisema.

DP alishambulia wapinzani wake na kuwataka kuacha kupuuza mfumo wake akisema ndio suluhu la kiuchumi.

Hawa watu wawache kiburi bwana…na wawache madharau…kazi ni kazi…kama ya Prime Minister ni kazi, ya hawa vijana ni kazi pia," alisema.

Alipigia debe Mbunge wa Thika Wainani Jungle kuchukua hatamu za uongozi wa kaunti hiyo kipindi kijacho.

Wakati wa ziara hiyo Ruto alipata mfuasi mpya baada ya aliyekuwa mbunge wa Thika Alice Ng'ang'a kujiunga na UDA.

Alisema ametabiri kuwa UDA ndiyo itaunda serikali ijayo na hivyo atawania ubunge wa eneo hilo kwa tiketi ya chama hicho.

"Muwaambie mama amerudi, sasa mimi ndio Ruto Defence Force. Tunamlinda mpaka Ikulu, na mimi nataka nichukue tena kiti ya mbunge," Alice alisema wakati wa ziara hiyo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke