Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto ana walinzi 257 wanaomlinda, Waziri Matiang'i asema

591606f5751931bb Ruto ana walinzi 257 wanaomlinda, Waziri Matiang'i asema

Wed, 1 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i amewahakikishia wabunge kuwa maisha ya Naibu Rais William Ruto hayamo katika hatari yoyote.

Matiang'i aliiambia Kamati ya Bunge ya Idara ya Utawala na Usalama wa Kitaifa kwamba Ruto ana maafisa wa usalama wa kutosha Aliongeza kwamba naibu rais wa sasa analindwa zaidi ikilinganishwa na watangulizi wake tangu enzi za uhuru Ruto anapewa ulinzi wa VVIP wa kikosi spesheli cha maafisa 74 wa kumlinda rais na maafisa wengine 183 kutoka idara mbali mbali.

Waziri huyo aliiambia Kamati ya Bunge ya Idara ya Utawala na Usalama wa Kitaifa kwamba Ruto ana walinzi wa kutosha ambao anapata kutoka kwa kikosi maalum kilichohitimu.

Alisema Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai alikuwa ameshauriana na idara za usalama kabla ya kufanya mabadiliko ya usalama katika makazi ya Ruto.

"Sisi hatumdhalilishi DP Ruto wala kufanyia mzaha usalama wake. Mpangilio huo ulianzishwa na IG kwa sababu ambazo siwezi kuelezea hapa hadharani. Tulimjulisha DP kuhusiana na mabadiliko hayo kwani ni jambo l kawaida kufanya hivyo," alisema.



Read also

Magazeti Jumatano: ODM Yakerwa na Wanjigi kwa Kumuita Raila Mzee

Alipowasili mbele ya kamati hiyo Jumatano, Septemba 1, alitoa taarifa zaidi kwamba naibu rais wa sasa analindwa zaidi ikilinganishwa na watangulizi wake tangu enzi za uhuru.

Wakati uo huo, Matiang'i alifafanua kwamba Rais Uhuru Kenyatta na Naibu Rais William Ruto, wanalindwa na vikosi tofauti chini ya kitengo spesheli cha rais.

Kulingana na Matiang'i, Ruto kwa sasa anapewa ulinzi wa VVIP wa kikosi spesheli cha maafisa 74 wa kumlinda rais ba maafisa wengine 183 kutoka idara mbali mbali wanaolinda makazi yake.

"Mbali na maafisa usalama wa urais 74 wanaomlinda DP, ana jumla ya maafisa 257 wanaolinda mali yake. Afisi ya naibu rais ina maafisa wa kutosha wa usalama," aliwaambia wakamati hao.

Wakati wa kikao hicho, Matinag'i pia alitoa orodha ya jumla ya maafisa wa usalama waliowalinda makamu wa rais wa zamani tangu enzi za uhuru.

Hii hapa ni historia ya maafisa wa usalama waliowalinda makamu wastaafu wa urais;

Read also

Magazeti Jumanne, Agosti 31: Uhuru Kuwapiga Kalamu Baadhi ya Marafiki Zake Mawaziri

1. Jaramogi Oginga Odinga - 30

2. Joseph Murumbi - 22

3. Daniel Moi - 34

4. Mwai Kibaki - 26

Josephat Karanja - 22

6. George Saitoti - 30

7. Musalia Mudavadi - 22

8. Kijana Wamalwa - 22

9. Moody Awori - 22

10. Kalonzo Musyoka - 26

11. William Ruto - 257

Mnamo Alhamisi, Agosti 26, Huduma ya Kitaifa ya Polisi ilibadilisha zaidi ya maafisa 70 wa GSU wanaolinda makazi ya Ruto na wenzao waliochukuliwa kutoka kitengo cha kulinda majengo ya serikali.

"Hili ni jambo la kawaida katika Huduma ya Kitaifa ya Polisi ili kuimarisha huduma za usalama. Kikosi spesheli cha kumlinda Rais kinaendelea kutoa ulinzi wa karibu kwa William Ruto," msemaji wa polisi Bruno Shioso alielezea.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Ruto Awakaribisha Walinzi Wake Wapya Nyumbani Kwake, Wanywa Chai Pamoja

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke