Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto amtembelea Jaguar hospitalini baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti

E490bc5f490f0628 Ruto amtembelea Jaguar hospitalini baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti

Thu, 1 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto alimtembelea mbunge huyo wa Starehe katika Hospitali ya Nairobi ambapo anaendelea kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa gotiJaguar alilazwa hospitalini humo baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye mguu wake wa kulia Ruto alikuwa ameandamana pamoja na wabunge wengine wakati wa ziara hiyo

Naibu Rais William Ruto, siku ya Jumatano, Juni 30, alimtembelea mbunge wa Starehe anayeugua Charles Njagua almaarufu Jaguar katika Hospitali ya Nairobi ambapo anaendelea kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.

Jaguar alilazwa hospitalini humo kwa uchunguzi zaidi wa kimatibabu baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye mguu wake wa kulia Jumanne, Juni 29.

Katika picha ambazo TUKO.co.ke imetazama, Ruto anaonyeshwa akizungumza na mbunge huyo aliyekuwa amelala kwenye kitanda cha wagonjwa.

Udukuzi kwenye kurasa za mtandao wa kijamii wa Jaguar unamuonyesa akijibu jumbe zilizochapishwa kwenye kurasa za mtandao wa kijamii kuhusu kutembelewa na Ruto.

Kulingana na mwanamuziki DK Kwenye Beat, ambaye alizungumza na gazeti moja nchini kuhusu hali ya Jaguar, alisema mbunge huyo amekuwa akikumbana na maumivi kwenye magoti yake kila mara licha ya kutafuta matibabu.

DK alisema mbunge huyo alisafiri hadi India kwa matibabu lakini bado tatizo hilo limekuwa likimsumbua.

Taarifa za kuaminika ziliarifu kwamba Jaguar aliumia goti lake kwenye vurugu iliyotokea kati ya wafanyabiashara wa masoko ya Muthurwa, Marikiti na Wakulima mwaka wa 2019.

Alilazwa katika Hospitali ya Karen ambapo alitibiwa na kuruhusiwa kuenda nyumbani.

Viongozi wengine walioandama na Ruto wakati wa ziara hiyo ni ikiwemo George Theuri (Mbunge Embakasi Magharibi), Mohammed Ali (Nyali), Korir Nixon (Lang’ata), John Kiarie (Dagoretti Kusini) na Yusuf Hassan (Kamukunji).

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke