Serikali ya Rais William Ruto wa Kenya inadaiwa kuanza uchunguzi wa Kampuni takriban 300 zinazohusishwa na kutolipa Kodi, baadhi yake zikimilikiwa na familia ya Rais msitafu wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta na watu waliowahi kuwa na Mamlaka katika Serikali zilizopita.
Waziri wa Fedha, Njuguna Ndung’u na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Kodi (KRA), Anthony Ng’ang’a Mwaura wamesema tayari wameanza ukagauzi wa kampuni ambazo zimekuwa zikipewa Misamaha ya Kodi kinyume cha Sheria.
Mama wa Kenyatta, Mama Ngina ameonesha kukerwa na kitendo cha familia yake kuhusishwa na Ukwepaji Kodi huku akitoa Onyo kwa Serikali isijaribu kuuza mali zake.