Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto aahidi kuwapa makahaba Tsh. Milioni 20 waanzishe biashara halali

Ac8710a566d18bed Ruto aahidi kuwapa makahaba Tsh. Milioni 20 waanzishe biashara halali

Tue, 26 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amewaahidi makahaba wa Makueni Tsh. milioni 20 kama mtaji wa kuanzisha biashara zenye heshima. Ruto aliwaomba kubuni chama ili aweze kuwapa pesa hizo akiahidi kusimama nao hadi biashara zao za heshima zitakapofaulu.

Naibu Rais amekuwa akitoa ahadi nyingi huku kampeni za 2022 zikipamba moto

Ruto ambaye alitumia muda wake Jumatatu, Oktoba 25, kupiga ziara nchini kuuza sera zake za kuwania urais mwaka 2022, alisikia kilio cha makahaba ambao walimuomba kuharakisha kutoa pesa za 'hazina ya kuwawezesha mahasla'.

Kwa mujibu wa Citizen TV, Ruto aliwaomba wabuni chama ili aweze kuwapa KSh 1 milioni za kuanzisha biashara nadhifu.

Ruto aliahidi kusimama nao hadi biashara zao za heshima zitakapofaulu.

Naibu Rais amekuwa akitoa ahadi nyingi huku kampeni za 2022 zikipamba moto.

Orodha ya CRB

Mnamo Jumamosi, Oktoba 24, Ruto aliahidi kuwasaidia mamilioni ya Wakenya ambao wako kwenye orodha ya shirika la kufuatilia wasiolipa mikopo (CRB) iwapo atachaguliwa kuwa rais 2022.

Ruto aliyetoa ahadi hiyo alipokuwa kwenye ziara ya Kiambaa, alisema kwamba anadhamiria kuwasaidia Wakenya waliolemewa na milima ya madeni ili waweze kujistawisha kifedha na kimaisha.

Ruto alisema serikali yake itatenga KSh 50 billioni kila mwaka kwa Wakenya milioni 14 ambao wamo kwenye orodha ya CRB.

"Kuna Wakenya milioni 14 ambao wako kwenye orodha ya CRB na ndiposa nimejitolea kutenga fedha za serikali zitakazorekebisha mfumo wa fedha ili nchi hii ikome kufanyia kazi watu wawili au watatu," Ruto alisema.

KSh 100M kwa vijanaWakati huo huo, Ruto alizungumzia kuhusu ahadi aliyotoa ya kuwapa vijana KSh 100 millioni chini ya vuguvugu lake la hasla.

Ruto alisema sawia na serikali ya Jubilee inavyotoa KSh 100 milioni za maendeleo kwa kila eneo bunge, naye pia atahakikisha kuwa mahasla wanapata pesa hizo kwa biashara zao punde atakapochukuwa hatamu za uongozi.

"Sawia na tunavyotenga KSh 100 milioni kwa kila eneo bunge kila mwaka za miradi ya maendeleo, raundi hii tutatenga KSh 100 milioni kila mwaka kusaidia watu kama mama mboga, wale ambao wanatumia wilibaro na mkokoteni," alisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke