Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ruto aahidi kulipa mikopo ya CRB akichaguliwa kuwa Rais

A60211766c60f0b6.png Ruto aahidi kulipa mikopo ya CRB akichaguliwa kuwa Rais

Mon, 25 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amesema iwapo atashinda kiti cha urais 2022, atawaokoa Wakenya waliowekwa kwenye orodha ya shirika la kufuatilia wasiolipa mikopo (CRB). Ruto amesema kwamba atatenga fedha za serikali zitakazo wakwamua Wakenya walioorodheshwa na shirika hilo ili wawe na uwezo wa kujisimamia tena.

Ruto aliwashukuru wakaaji wa Kiambaa kwa kumpigia kura na kumchagua Njuguna Wanjiku, kuwa mbunge wa kwanza wa chama cha UDA Naibu Rais William Ruto ameahidi kuwasaidia mamilioni ya Wakenya ambao wako kwenye orodha ya shirika la kufuatilia wasiolipa mikopo (CRB) iwapo atachaguliwa kuwa rais 2022.

Ruto aliyetoa ahadi hiyo alipokuwa kwenye ziara ya Kiambaa, alisema kwamba anadhamiria kuwasaidia Wakenya waliolemewa na milima ya madeni ili waweze kujistawisha kifedha na kimaisha.

Akizungumza mnamo Jumapili, Oktoba 24, katika eneo bunge hilo, Ruto alisema serikali yake itatenga KSh 50 billioni kila mwaka kwa Wakenya milioni 14 ambao wamo kwenye orodha ya CRB.

"Kuna Wakenya milioni 14 ambao wako kwenye orodha ya CRB na ndiposa nimejitolea kutenga fedha za serikali zitakazorekebisha mfumo wa fedha ili nchi hii ikome kufanyia kazi watu wawili au watatu," Ruto alisema.

Ahadi kwa vijana Kufikia mwezi wa Februari mwaka huu, Wakenya milioni 14 wenye madeni ya takriban KSh 423 billioni, waliorodheshwa na CRB kwa kushindwa kulipa mikopo. Wakati huohuo, Ruto alizungumzia kuhusu ahadi aliyotoa ya kuwapa vijana KSh 100 millioni chini ya vuguvugu lake la hasla.

Ruto aliwashukuru sana wenyeji wa Kiambaa kwa kumchagua mbunge wa kwanza wa chama cha United Democratic Movement (UDA), Njuguna Wanjiku.

"Kwa sababu mlimchagua Kawanjiku, sasa tuna wabunge 155 kutoka chama cha UDA," Ruto alisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke