Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ronaldo apigwa marufuku kwa kuvua shati kusherehekea kuvunja rekodi ya kimataifa

12c2a25b24970c85 Ronaldo apigwa marufuku kwa kuvua shati kusherehekea kuvunja rekodi ya kimataifa

Thu, 2 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Cristiano Ronaldo alilishwa kadi ya manjano akisherehekea bao lake la ushindi dakika za lala salama dhidi ya Ireland wakati wa mechi ya kufuzu kwa Kombe la DuniaAdhabu hiyo itamshuhudia akikosa ziara ya Ureno kuelekea Azerbaijan lakini atakuwa katika mechi ya kirafiki Qatar Ronaldo hababaishwi na adhabu hiyo huku akiweka rekodi ya kihistoria dhidi ya Ireland Cristiano Ronaldo hatashiriki mechi ijayo ya kufuzu kwa Kombe la Dunia ya Ureno dhidi ya Azerbaijan ambayo imeratibiwa kuchezwa Jumanne, Septemba 10.

Hii ni baada ya sajini huyo mpya wa Man United kuvua shati yake akisherehekea magoli yake mawili usiku wa Jumatano, Septemba 1.

Bao lake la pili lilimsaidia Ronaldo kuvunja rekodi ya kimataifa ya mfungaji wa mabao mengi duniani na hivyo alivua shati yake kusherehekea hatua hiyo.

Hata hivyo, hatua hiyo ilimpelekea kupokea kadi ya manjano kutoka kwa refa wa Slovenia, Matej Jug, ambaye alimuomba msamaha akichomoa kadi hiyo.

Sunsport inaripoti kuwa adhabu hiyo itamshuhudia akikosa ziara ya Ureno kuelekea Azerbaijan lakini atakuwa katika mechi ya kirafiki Qatar.



Ronaldo avunja rekodiLicha ya kuadhibiwa, Ronaldo hababaishwi na adhabu hiyo huku akiweka rekodi ya kihistoria dhidi ya Ireland.

Kabla ya mechi hiyo ya Ureno dhidi ya Ireland, mshindi huyo mara tano wa Ballon d'Or alikuwa anatoshana na bingwa wa Iran, Daei na magoli 109.

Fowadi huyo wa United alichukuwa fursa ya mapema kuongezea jumla ya mabao yake kuwa 110 wakati alipoteza penalti.

Hata hivyo, alijirekebisha akifunga magoli mawili dakika za mwisho ikiwemo moja katika dakika ya 89, akichuma nafuu kutoka kwa krosi ya Goncalo Guedes.

Bao hilo la ushindi liliongezea jumla ya magoli yake kuwa 111 kimataifa ambayo ni rekodi mpya.

"Ninafuraha sana, sio kwa sababu nimevunja rekodi, bali kwa muda wa maalum ambao tulikuwa nao. Magoli mawili katika mwisho wa mchezo. Ninapaswa kushukuru kile ambacho timu ilifanya. Tulikuwa na imani mpaka mwisho. Nimefurahi sana," alinukuliwa Ronaldo akizungumza baada ya kuvunja rekodi hiyo.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke