- Nzembi alitoweka Jumamosi, Mei 29, baada ya kuondoka nyumbani kwenda kucheza na marafiki zake
- Mtaalamu mkuu wa upasuaji wa maiti Kenya Johansen Oduor alisema mwanafunzi huyo wa darasa la Pili wa miaka nane alifariki dunia baada ya kunyongwa
- Sampuli zaidi zilichukuliwa kwa ukaguzi wa kina ili kubaini iwapo waliomteka nyara walimdhulumu
Uchunguzi wa maiti uliofanywa kwenye mwili wa msichana wa Kitengela wa miaka minane umebaini alifariki dunia kutokana na kukosa hewa.
Haya ni kwa mujibu wa mtaalamu mkuu wa upasuaji wa maiti nchini Kenya daktari Johansen Oduor.
Oduor ambaye alifanya upasuaji huo katika hospitali ya Shalom Community mnamo Ijumaa, Juni 4 alisema kuwa Shantel Nzambi alizibwa mdomo na mapua ambapo alishindwa kupumua.
Sampuli zaidi zilichukuliwa kwa ukaguzi wa kina ili kubaini iwapo waliomteka nyara walimdhulumu kama jinsi baadhi ya ripoti zilisema.
Nzembi alipotea Jumapili alasiri, Mei 30, alipoondoka nyumbani kwenda kucheza na rafiki yake aliyejulikana kama Sharon, ambaye ni bintiye afisa wa polisi.
Mamake, Christine Ngina ambaye alikuwa amegubikwa na majonzi alisimulia jisni alivyopokea simu kutoka kwa mwanamke aliyedai pesa ili amwachilie Nzembi.
"Nilipokea simu nyingi. Mwanzo walinipigia simu Jumamosi na kila mara walikuwa wakiniuliza iwapo nimepata pesa. Sielewi ni kwa ni nini hawakuwa na subra," alisema.
Kufikia sasa, polisi wamewakamata washukiwa watatu akiwemo Nativity Mutindi, 30, ambaye alifumaniwa mafichoni Athi River Ijumaa, Juni 4.
Haya yalijiri siku chache baada ya mahakama Kajiado kuamuru washukiwa wengine wawili, Livingstone Makacha Otengo na Francis Mbuthia Mikuhu, wazuiliwe kwa siku 10 ili wapelelezi wakamilishe uchunguzi.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.