Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) limesema theluthi moja tu ya Watoto chini ya miaka miwili katika Nchi zinazoendelea hupata Chakula wanachohitaji kwa ukuaji bora.
Ripoti ya UNICEF imesema, majanga mbalimbali ikiwemo ghasia, mafuriko, mlipuko wa ugonjwa wa Corona na mabadiliko ya Tabia Nchi yamekwamisha Maendeleo ya lishe kwa Watoto katika Mataifa 91.
Watoto waishio katika mataifa yanayokumbwa na majanga wanapitia changamoto kubwa katika ukuwaji wao. kwa sasa nchini Burundi watoto wengi wanapitia wakati mgumu kufuati mafuriko yaliyo poteza makazi mengi ya wananchi. na kupelekea kuishi kwenye kambi za msaada.
Majanga yananayozikumba nchi zinazoendelea huatarisha maisha ya watoto kwa kukosa mahitaji muhimu ikiwemo mlo kamili hali ammbayo imepelekea Afya za watoto kuzorota.