Wananchi wa Tunisia wanatarajiwa kupigia Kura ya Maoni Rasimu ya Katiba Mpya ambayo wakosoaji wa Rais Kais Saied wanahofia itaua Demokrasia iliyopatikana kufuatia Mapinduzi ya Mwaka 2011
Rasimu hiyo imepingwa na Vyama vya Siasa pamoja na Asasi mbalimbali za Kiraia kwa madai inamuongezea Rais Mamlaka makubwa, na hivi karibuni yamekuwepo Maandamano ya kutoiunga mkono
Kwa mujibu wa Taratibu alizoweka Rais Saied, hakuna kiwango cha chini cha ushiriki kinachohitajika kuidhinisha Katiba hiyo itayoanza kutumika mara tu matokeo ya mwisho yakichapishwa. Haijawekwa wazi nini kitatokea ikiwa Wapiga Kura wataikataa