Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ramaphosa anakabiliwa na tishio la kushtakiwa kwa kashfa ya kuwahonga wezi

C6bc12ce 49c0 41c5 A0e3 05af5d95d6f5 Ramaphosa anakabiliwa na tishio la kushtakiwa kwa kashfa ya kuwahonga wezi

Thu, 1 Dec 2022 Chanzo: Bbc

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anakabiliwa na tishio la kuondolewa madarakani kwa kura ya kutokuwa na Imani naye kutokana na kashfa ya kuwahonga wezi.

Rais ameshutumiwa kwa kuficha wizi wa $4m (£3.3m) kutoka kwa shamba lake mnamo 2020, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara na kuwahonga wezi hao kimya.

Ripoti iliyofichuliwa kutoka kwa jopo huru imegundua kuwa Bw Ramaphosa alitumia vibaya nafasi yake na huenda alivunja sheria ya kupambana na ufisadi.

Hata hivyo, rais huyo amekana kufanya makosa, na kusema pesa hizo zilitokana na kuuza nyati.

Matokeo ya jopo hilo yamekabidhiwa bunge ambalo linatazamiwa kuyachunguza na kuamua iwapo litaanzisha mchakato wa kujadiliwa kwa hoja hiyo au la wiki ijayo.

Bw Ramaphosa amesalia chini ya mwezi mmoja kabla ya kongamano litakaloamua iwapo anaweza kuwania muhula wa pili na chama chake, African National Congress (ANC), mwaka wa 2024.

Tukio hilo linaweza kuwa mbaya zaidi huku Bw Ramaphosa akiwania wadhifa huo.

ANC itafanya mkutano na watendaji wake siku ya Alhamisi, ambapo inatarajiwa kuwa suala hilo litajadiliwa.

Kashfa ya Farmgate ilizuka mwezi Juni, wakati mkuu wa zamani wa jasusi wa Afrika Kusini, Arthur Fraser, alipowasilisha malalamiko kwa polisi akimshtumu rais kwa kuficha wizi wa $4m kutoka kwa shamba lake la Phala Phala kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo mnamo 2020.

Bw. Fraser, ambaye ni mshirika wa karibu wa Rais wa zamani Jacob Zuma, alidai kuwa pesa hizo zingeweza kuwa mapato ya utakatishaji fedha na ufisadi, na kumshutumu rais kwa kuwateka nyara na kuwahonga wezi hao.

Kushikilia kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa dola kunaweza kukiuka sheria za udhibiti wa fedha za kigeni.

Bw Ramaphosa amethibitisha kuwepo kwa wizi, lakini akasema kiasi kilichoibiwa kilikuwa kidogo kuliko kile kinachodaiwa, na akakana kujaribu kuficha.

Chanzo: Bbc