Katika hotuba yake Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema Hayati Dk John Magufuli alisimama kama shujaa dhidi ya rushwa na ubadhirifu.
Alimuelezea Dk Magufuli kama kiongozi aliyepinga vitendo hivyo akiamini viongozi wanapaswa kutumikia wananchi wao
Amemshukuru Dk Magufuli kwa kuelekeza nguvu katika maendeleo ya kiuchumi wa Taifa la Tanzania, Ukanda na Bara la Afrika kwa ujumla
Vilevile, Rais Ramaphosa amemshukuru Hayati Dk Magufuli kwa kuwa Mwana wa Afrika aliyeona umuhimu wa tamaduni kukumbukwa na kufundishwa, akisema alikuwa Kiongozi aliyetaka watu kujivunia Lugha za Kiafrika
Amesema Tanzania ilipata bahati kuwa na Kiongozi kama Hayati Dk John Magufuli.