Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa zamani wa Zambia Kenneth Kaunda, 97, alazwa hospitalini

2fed3b1875ed855b Rais wa zamani wa Zambia Kenneth Kaunda, 97, alazwa hospitalini

Tue, 15 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Anapokea matibabu ya ugonjwa ambao haujatajwa katika hospitali ya jeshi jijini Lusaka, ofisi yake imesema

- Kaunda alitawala Zambia kutoka 1964 hadi 1991, wakati taifa hilo la Kusini mwa Afrika lilipopata uhuru wake kutoka kwa Uingereza na ni miongoni mwa mashujaa wachache wa ukombozi wa bara hili ambao bado wanapumua

- Rais Edgar Lungu alihimiza taifa kumuombea rais huyo wa zamani ili "Mungu amguse kwa mkono wake wa uponyaji"

Aliyekuwa Rais wa Zambia Kenneth Kaunda, 97, anapokea matibabu ya ugonjwa ambao haujatajwa katika hospitali ya jeshi jijini Lusaka, ofisi yake imesema.

Kaunda alitawala Zambia kutoka 1964 hadi 1991, wakati taifa hilo la Kusini mwa Afrika lilipopata uhuru wake kutoka kwa Uingereza. Yeye ni miongoni mwa mashujaa wachache wa ukombozi wa bara hili ambao bado wanapumua.

Mpambe wake wa utawala Rodrick Ngolo alisema Jumatatu, Juni 14, katika taarifa kwamba Kaunda amekuwa akihisi maumivu na amelazwa katika Kituo cha Matibabu cha Maina Soko huko Lusaka.

"Ofisi na familia ya rais wa kwanza zinataka kuarifu umma kwa ujumla kwamba Mheshimiwa Dkt Kenneth D. Kaunda, rais wa kwanza wa Zambia amekuwa mgonjwa na amelazwa hospitalini katika Kituo cha Matibabu cha Maina Soko," taarifa ya Ngolo ilisema.

"Mheshimiwa Dkt Kaunda anawaomba Wazambia wote na jamii ya kimataifa wamuombee kwani timu ya matibabu inafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa anapona." iliongeza kusema.

Rais Edgar Lungu alihimiza taifa kumuombea rais huyo wa zamani ili "Mungu amguse kwa mkono wake wa uponyaji".

"Alilitetea taifa hili kubwa wakati wake muhimu zaidi, na kwa hivyo tunaweza wote kumtetea wakati wake wa udhaifu," Lungu alisema kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama video kemkem za kusisimua TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke