Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa zamani wa Sierra Leone anayekabiliwa na mashtaka ya uhaini aruhuisiwa kusafiri

Rais Wa Zamani Wa Sierra Leone Anayekabiliwa Na Mashtaka Ya Uhaini Aruhuisiwa Kusafiri Rais wa zamani wa Sierra Leone anayekabiliwa na mashtaka ya uhaini aruhuisiwa kusafiri

Thu, 18 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Rais wa zamani wa Sierra Leone amepewa ruhusa ya kusafiri nje ya nchi kwa matibabu licha ya kukabiliwa na mashtaka ya uhaini.

Uamuzi huo wa Mahakama Kuu unakuja huku kukiwa na uvumi kwamba Ernest Bai Koroma amekubali kwenda uhamishoni nchini Nigeria ikiwa mashtaka dhidi yake yatafutwa.

Alishtakiwa kwa uhaini na makosa mengine juu ya mapinduzi yaliyoshindwa Novemba mwaka jana, ambapo watu 20 walikufa.

Bw Koroma, ambaye alitawala kati ya 2007 na 2018, anakanusha madai haya.

Amri ya mahakama ambayo BBC iliona Jumatano inaonyesha Bw Koroma anaruhusiwa kusafiri hadi Nigeria kwa sababu za kimatibabu.

Amri hiyo inasema kwamba hapaswi kukaa huko kwa zaidi ya miezi mitatu na kwamba lazima afike mbele ya mahakama ya hakimu ya Sierra Leone tarehe 6 Machi.

Wakati wa shambulio la mwaka jana,watu wenye silaha walivamia ghala la silaha la kijeshi na magereza kadhaa katika mji mkuu wa Freetown, na kuwaachilia karibu wafungwa 2,000.

Serikali ilieleza kuwa jaribio hilo la mapinduzi na mapema mwezi huu, Bw Koroma alishtakiwa pamoja na washukiwa wengine 12.

Vyanzo visivyojulikana kutoka Umoja wa Mataifa na Ecowas, muungano wa nchi za Afrika Magharibi, viliambia BBC kwamba Ecowas ilikuwa imepanga mpango wa Bw Koroma kwenda uhamishoni nchini Nigeria ikiwa mashtaka yatafutwa.

BBC pia iliona barua ikisema Bw Koroma amekubali mpango huo, ambao utamfanya aendelee kufurahia marupurupu ya rais wa zamani hata akiwa Nigeria.

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Sierra Leone Timothy Kabba hapo awali aliiambia BBC kuwa serikali haikuunga mkono pendekezo hilo, ambalo alilitaja kama "pendekezo la upande mmoja" la rais wa Tume ya Ecowas.

Ecowas imekuwa na wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa mvutano nchini Sierra Leone kufuatia jaribio la mapinduzi.Katika miaka ya 1990 Ecowas ilishuhudia kwa karibu maafa ya vita vya kikatili vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi na kutuma kikosi cha kulinda amani kusaidia kumaliza mzozo huo.

Baadhi ya wanadiplomasia wanaamini Bw Koroma hatarejea kutoka Nigeria baada ya kusafiri huko kwa misingi ya matibabu na kwamba amri ya mahakama inamruhusu kwenda uhamishoni kama njia ya kurejesha utulivu nchini humo.

Bw Koroma alikuwa rais kwa miaka 11 hadi 2018, wakati Rais wa sasa Julius Maada Bio alipochaguliwa.

Chanzo: Bbc