Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa zamani wa Burundi afariki dunia

SEM Pierre BUYOYA Haut Representant CUA 660x400 Rais wa zamani wa Burundi afariki dunia

Sat, 19 Dec 2020 Chanzo: millardayo.com

Rais wa zamani wa Burundi Pierre Buyoya amefariki akiwa na umri wa miaka 71, binamu yake na chanzo cha kidiplomasia kimethibitishia taarifa za kifo chake.

Chanzo cha familia kimesema amefariki Mjini Paris, Ufaransa siku ya Alhamisi kutokana na athari za ugonjwa wa Covid-19.

Jenerali huyo mstaafu alihudumu mara mbili madarakani kwa jumla ya miaka 13 baada ya kumpindua mtangulizi wake madarakani

Mwezi October, alihukumiwa kifungo cha maisha gerezani na Mahakama ya Burundi kwa kosa la mauaji ya rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini humo, Rais Melchior Ndadaye mwaka 1993 -ambayo yalisababisha mauaji ya karibu watu 300,000. Alikana kufanya makosa hayo.

Chanzo: millardayo.com