Rais Edgar Chagwa Lungu alikuwa buheri wa afya Jumapili, Juni 13, wakati aliongoza hafla ya kumbukumbu ya 45 ya Jeshi la Ulinzi la ZambiaHata hivyo, akiwa katika hafla hiyo ya jeshi, rais huyo anadaiwa kuhisi kisunzi ghafla na kumpelekea kuziraiAlipata fahamu haraka na kuelekea moja kwa moja kwenye gari lake na kurejea Ikulu ambapo amekuwa akikagua vidimbwi vya samaki
Ripoti kutoka Zambia zinadai kuwa rais wa taifa hilo Edgar Chawga alizirai Jumapili, Juni 13, akiongoza hafla ya kumbukumbu ya 45 ya Jeshi la Ulinzi jijini Lusaka.
Taarifa ya Waziri Simon Miti ilidai kuwa rais huyo alikumbana na kisunzi wakati wa hafla hiyo lakini alipata fahamu haraka na kuelekea moja kwa moja kwenye gari lake na kurejea Ikulu.
Miti alibainisha kuwa kiongozi huyo yuko katika hali nzuri na anaendelea kuchapa kazi.
Baada ya udukuzi kwenye ukurasa wake wa Facebook, TUKO.co.ke ilitambua rais huyo akionyeshwa mubashara kutoka Ikulu akikagua vidimbwi vya samaki.
Hafla hiyo ya kumbukumbu ilichukua muda wa saa nne pekee huku Lungu akitumia fursa hiyo kuwapongeza na kuwasifu wanajeshi kwa kujitolea kutumikia taifa la Zambia.
"Kwa miaka kadhaa uzalendo wenyu kwa taifa hili haujakuwa wa kutiliwa shaka, ninajua mtapepea juu ya siasa ili kutetea taifa hili dhidi ya athari yoyote kwa amani na usalama. Ninawapigia saluti kwa kujitolea kwenyu na uzalendo wenyu kwa taifa hili," alisema Lungu.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.