Tue, 31 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amesema serikali yake haihamasishi haki za wapenzi wa jinsia moja, tovuti ya Lusaka Times imeripoti, ikinukuu matamshi yake katika ibada ya kanisa.
Nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ni moja ya nchi ambazo vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ni kinyume cha sheria.
Rais anaripotiwa kuwaambia waumini kwamba msimamo wake kuhusu haki za wapenzi wa jinsia moja haujabadilika tangu akiwa upinzani.
Aliwataka Wazambia "kutozingatia mambo ambayo hayana umuhimu".
Katiba ya Zambia inaitambulisha nchi hiyo kuwa ya Kikristo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live