Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa Zambia Edga Lungu akubali matokeo ya uchaguzi, ampongeza mpinzani wake

F7d739c9fa09bcc5 Rais wa Zambia Edga Lungu akubali matokeo ya uchaguzi, ampongeza mpinzani wake

Tue, 17 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais anayeondoka wa Zambia Edga Lungu amekubali kushindwa katika uchaguzi mkuu uliokamilika hivi majuziHakainde Hichilema ambaye alikuwa mpinazani wake mkuu, alimbwaga rais huyo kwa kuzoa kura 2,810,757 dhidi ya Edgar Lungu aliyepata kura 1,814,201 Hata hivyo, Lungu alikuwa amepinga matokeo hayo hapo awali akidai kura ziliibiwaHalaiki ya wafuasi wa Hakainde walijitokeza katika mitaa ya jiji la Lusaka kusherehekeaRais anayeondoka wa Zambia Edga Lungu amekubali kushindwa na kumpongeza mpinzani wake mkuu Hakainde Hichilema ambaye aliibuka mshindi wa uchaguzi mkuu.

Kwenye hotuba yake kwa taifa, Raia Lungu alikuwa na haya ya kusema,"

" Ningependa kumpongeza kakangu Hichielema kwa kuwa Rais wa saba wa nchi hii, namtakia heri njema anapochukua hatamu za uongozi, " Alisema Lungu.

Lungu alisema atakubaliana na katiba kuhusu ubadilishanaji wa mamlaka.

Rais huyo alichukua hatamu za uongozi mwaka wa 2015 kutoka kwa mtangulizi wake Michael Sata ambaye alifariki dunia akiwa bado afisini.

" Ningependa kuwashukuru wananchi wa Zambia kwa kunipa fursa kuwa rais wao, milele nitajivunjia na kuthathimini utawala mlioowekeza ndani yangu, Kile nilichokitaka ni kuhudumia nchi yangu kadri ya uwezo wangu ingawa kulikuwa na changamoto si haba," Alisema Lungu.



Baada ya Hakainde kujaribu mara tano bila ufanisi, rais huyo mteule alishinda katika jaribio lake la sita na pia ilikuwa mara yake ya tatu kupambana Lungu.

Hakainde Hichilema alizoa kura 2,810,757dhidi ya Lung ambaye alipata kura 1,814,201.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, Lungu alikuwa ametishia kuchukua hatua za kisheria kupinga matokeo hayo akidai yalizingirwa na wizi wa kura.

Kando na hayo, hapa Kenya siasa za uchaguzi mkuu wa 2022 zimeshika moto huku Rais Uhuru Kenyatta akidokeza kwamba atamuidhinisha kinara wa chama cha ODM Raila Odinga kuwa mrithi wake.

Madai hayo yameibua hisia mseto miongoni mwa Wakenya huku Naibu Rais William Ruto akiendelea kupiga kampeni zake akiwa na matumaini kwamba ifikapo 2022 atakuwa ikulu.

Raila amewania urais kwa mara 5 bila mafanikio, wafuasi wake wamempa mfano wa Rais Lungu wakisema pia yeye huenda akafanikiwa 2022.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke