Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa Somalia aapa kulitokomeza kundi la Al Shabab

Somalia Rais Rais wa Somalia aapa kulitokomeza kundi la Al Shabab

Wed, 24 Aug 2022 Chanzo: VOA

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud Jumanne ameahidi vita vikali kutokomeza kundi la Al Shabab katika taarifa yake ya kwanza kwa taifa tangu wanamgambo hao wa Kiislamu kufanya uvamizi mbaya wa saa 30 kwenye hoteli moja mjini Mogadishu.

Shambulio hilo ambalo lilianza Ijumaa jioni, lilikuwa ndilo kubwa zaidi kukumba mji mkuu wa Somalia tangu Mohamud aingie madarakani mwezi Juni na kusisitiza changamoto ya kujaribu kumaliza uasi wa miaka 15 wa kundi lenye uhusiano na Al-Qeada.

Watu 21 walifariki na wengine 117 kujeruhiwa katika shambulio hilo la bunduki na mabomu lililolenga hoteli maarufu ya Hayat, na raia wa Norway ni miongoni mwa waliokufa, kwa mujibu wa serikali ya Norway.

“Ninajua kwamba wanainchi wa Somalia wamechoshwa na rambirambi na maombolezo yasiyoisha, najua kwamba mnawapoteza watu wenye thamani katika kila shambulio linolafanywa na magaidi,” Mohamud amesema.

“Tuna dhamira ya kuwadhoofisha magaidi wanaoteketeza wanainchi wetu hadi maeneo yote wanayoyadhibiti yamekombolewa, hili ni jambo la kipaumbele kwa serikali yetu na maandalizi na utelekelezaji wa mpango huo unaendelea,” amesema bila kufafanua zaidi.

Chanzo: VOA