Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa Senegal atangaza tarehe ya uchaguzi wa mwezi huu

Rais Wa Senegal Atangaza Tarehe Ya Uchaguzi Wa Mwezi Huu Rais wa Senegal atangaza tarehe ya uchaguzi wa mwezi huu

Thu, 7 Mar 2024 Chanzo: Bbc

Serikali ya Senegal imetangaza kuwa uchaguzi wa rais wa nchi hiyo utafanyika tarehe 24 Machi.

Tangazo hilo linafuatia hali ya mvutano nchini humo baada ya Rais Macky Sall kuahirisha uchaguzi mwezi uliopita, na hivyo kuzua maandamano makubwa.

Rais, ambaye muhula wake unamalizika tarehe 2 Aprili, alikuwa amesisitiza kwamba hakunuia kugombea muhula wa tatu madarakani.

Wapinzani wake walikuwa wamemshutumu kwa kuandaa mapinduzi ya kikatiba.

Senegal imeonekana kwa muda mrefu kama mojawapo ya nchi zenye demokrasia imara zaidi barani Afrika.

Ni nchi pekee katika Afrika Magharibi ambayo haijawahi kuwa na mapinduzi ya kijeshi.

"Rais wa Jamhuri aliarifu Baraza la Mawaziri kwamba tarehe ya uchaguzi wa urais ilikuwa imepangwa Jumapili Machi 24," baraza la mawaziri lilisema katika taarifa.

Kabla ya tangazo la Jumatano, viongozi walikuwa wamejaribu kuahirisha uchaguzi wa awali wa Februari 25 hadi Desemba, ambao ulisababisha machafuko mabaya mitaani.

Lakini Baraza la Katiba baadaye liliamua kwamba uchaguzi wa urais lazima ufanyike kabla ya tarehe 2 Aprili.

Mapema Jumatano jioni, Bw Sall alivunja serikali na kumweka Waziri Mkuu Amadou Ba na Waziri wa Mambo ya Ndani Sidiki Kaba.

Hii ilikuwa ili Bw Ba, mgombea urais wa muungano tawala, aweze kuzingatia kampeni yake ya uchaguzi, ofisi ya rais ilisema.

Rais Sall amehudumu kwa mihula miwili kama kiongozi wa Senegal na alipochaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2012 aliahidi kuwa hatakaa kwa muda mrefu.

Chanzo: Bbc