Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa Ghana amshawishi nyota wa Chelsea Hudson-Odoi abadilishe uraia

2cebfa6b8fb65f0f Rais wa Ghana amshawishi nyota wa Chelsea Hudson-Odoi abadilishe uraia

Wed, 9 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Callum Hudson-Odoi kwa sasa yuko nchini Ghana kwa likizo baada ya kukamilisha kampeni ya msimu wa 2020/21 vyema

- Mshindi huyo wa Ligi ya Mabingwa alikutana na rais wa taifa hilo Nana Akufo-Addo ambaye alimuagiza waziri wa michezo kuhakikisha kuwa mwanasoka huyo anabadilisha uraia wake

- Hudson-Odoi ambaye ameshikirikishwa mara tatu kwenye timu ya Three Lions of England aliondolewa na Gareth Southgate kwenye kikosi cha Euro 2020

Kuna wito kwa mchezaji nyota wa Chelsea Callum Hudson-Odoi kubadilisha uraia wake na kuchezea Ghana katika hadhi ya kimataifa.

Callum Hudson-Odoi mwenye umri wa miaka 20, kwa sasa yuko nchini Ghana kwa likizo baada ya kukamilisha kampeni ya msimu wa 2020/21 vyema

Winga huyo alikuwa sehemu ya kikosi cha Chelsea ambacho kilipiga Manchester City 1-0 katika fanaili ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) na kutawazwa mabingwa wa Ulaya.

Kutua kwake jijini Accra kuliyeyusha nyoyo za wafuasi huku wengi wakimuomba abadilishe uraia na kuchezea taifa la baba yake.



Baba yake Bismark Odoi alikuwa nguli katika mabingwa wa Ligi ya Ghana, Hearts of Oak miaka ya 90 kabla ya kuhamia Uingereza.

Hudson-Odoi ameshikirikishwa mara tatu kwenye timu ya Three Lions of England lakini kufuatia kubadilsuhwa kwa sheria za FIFA, bado nyota huyo anaweza kuchezea Ghana katika kipute cha AFCON.

“Jumatatu, Juni 7, 2021, mchezaji wa Chelsea mwenye mzawa wa Ghana, Callum Hudson-Odoi, alinitembelea katika Jumba la Jubilee House," rais Akufo-Addo alisema.

“Miongoni mwa wengine, nilimuhimiza waziri wa michezo amshawishi Callum abadilishe uraia na achezee Black Stars," aliongezea.

TUKO.co.ke iliripotia awali kuwa Chelsea wanajiandaa kumuweka mnadani Callum Hudson-Odoi katika dirisha la uhamisho la msimu ujao.

Callum Hudson-Odoi amepungukiwa kimchezo ugani Stamford Bridge chini ya uongozi wa Thomas Tuchel.

Metro UK inaripoti kuwa kinda huyo ana hamu ya kushirikishwa katika timu ya kwanza lakini yaonekana kuwa vigumu uwanjani Stamford Bridge kwani Tuchel anawapendelea wachezaji wengine.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke