Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais wa Burundi miongoni mwa viongozi walioalikwa kuhudhuria sherehe za Madaraka

C3f40cb4e9313693 Rais wa Burundi miongoni mwa viongozi walioalikwa kuhudhuria sherehe za Madaraka

Fri, 28 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Sikuu kuu ya Madaraka husherehekewa kila mwaka tarehe mosi mwezi wa Juni, hii ni tarehe ambayo Kenya ilipata uhuru mwaka wa 1963

- Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuongoza sherehe ya mwaka huu ya madaraka itakayofanyika katika uwanja mpya wa michezo wa Jomo Kenyatta Sports Complex mjini Kisumu

- Sherehe hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na watu 3,000 pekee na ambao watakuwa na kadi za mwaliko, miongioni mwao ni Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye

- Kulingana na gavana wa Kisumu Anyang' Nyong'o, masharti ya kudhibiti na kuzuia maambukizi ya Covid- 19 yatazingatiwa kwa kina

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye ni miongoni mwa wageni wachache waheshimiwa ambao wamealikwa kuhudhuria sherehe za siku kuu ya Madaraka mjini Kisumu Jumanne, Juni mosi.

Ndayishimiye huenda akawa kiongozi wa kipekee kutoka nchi za kigeni kuhudhuria sherehe hiyo kulingana na masharti ya Covid- 19.

Kwa mujibu wa taarifa za The Standard, Rais Ndayishimiye anatarajiwa kutua nchini Jumatatu Mei 31 kwa ajili ya kujiandaa kwa sherehe hiyo siku ya Jumanne.

Gavana wa Kisumu Anyang' Nyong'o alitangaza Alhamisi, Mei 27 kwamba wageni 3,000 pekee ndio wanatarajiwa kuhudhuria sherehe hiyo, hii ni kulingana na masharti ya COVID-19.

"Uwanja wa Jomo Kenyatta International una uwezo wa kushikilia zaidi ya watu 30,000 lakini tumewaalika 3, 000 pekee, hiyo ikiwa ni asilimia 10% ya idadi hiyo," Nyong'o alisema.

" Wale ambao amealikwa watahitajika kuja na kadi za mwaliko na viti vyao vimepangwa kwa umbali wa mita moja," Alisema Nyong'o.

Nyong'o amwahakikishia Wakenya kwamba masharti yote ya kuzuia maambukizi ya virusi vya COVID-19 yaliowekwa na wizara ya afya yatazingatiwaipasavyo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke