Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais mstaafu Mahakamani kwa utakatishaji fedha

5332A7A3 7D85 41E1 A55D EC82B14DB9BF.jpeg Rais mstaafu Mahakamani kwa utakatishaji fedha

Sat, 31 Dec 2022 Chanzo: dar24.com

Serikali ya Botswana, imetoa waranti wa kukamatwa kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo, Ian Khama akikabiliwa na mashtaka 14 ya uhalifu ikiwemo kumiliki silaha kinyume cha sheria na utakatishaji wa fedha.

Mara baada ya kupata taarifa hizo, Khama ambaye inasemekana kuwa yupo nchini Afrika Kusini amekanusha mashtaka dhidi yake, akisema ni ya uongo na kwamba yamechagizwa na masuala ya kisiasa.

Khama ambaye alijiuzulu mwaka 2018 baada ya kuhudumu kwa kipindi cha miaka 10, alikosana na mrithi wake, Mokgweetsi Masisi, ambaye amemshutumu kwa kutawala kimabavu.

Hata hivyo, Aprili 2022 Khama alidai anajihisi yuko salama akiwa Afrika Kusini na huenda kamwe asirejee Botswana, huku akikanusha madai ya kuukimbia mkono wa sheria na inaarifiwa kuwa iwapo Mahakama itamkuta na hatua anaweza tumikia kifungo cha  miaka 10 gerezani.

Chanzo: dar24.com