Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais mstaafu Jakaya Kikwete aseme angelipenda Magufuli akamilishe muhula wake

396e55f9ca82c86a Rais mstaafu Jakaya Kikwete aseme angelipenda Magufuli akamilishe muhula wake

Fri, 26 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Aliyekuwa Rais wa nne wa Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete amesema kifo cha mwenzake Hayati John Pombe Magufuli ni pigo kubwa kwake na hata kwa nchi kwa jumla.

Kikweti alisema alipokea habari za kifo cha Magufuli kwa mshtuko na hata hangetaka kukubali kwamba kingozi huyo hayupo tena.

Akizungumiza kuhusu uhusiano wake na Magufuli, Kikwete alisema Hayati alikuwa jembe lake wakati alipokuwa waziri katika serikali yake.

"Nilipokuwa Rais, Hayati Magufuli alikuwa Waziri wangu kwa miaka 10, alikuwa mmoja wa mawaziri niliowaamini zaidi na kumtumaini sana," Kikwete alisema.

“Ilikuwa ni matarajio yangu, kuwa rais wangu John Pombe Magufuli angekimaliza kipindi chake cha uongozi salama na kustaafu,

‘’Kwa kifupi Magufuli alikuwa jembe langu ndio maana nilimuweka kwenye wizara tatu zilizokuwa ngumu ili anyooshe Watanzania ukakamavu na utendakazi wake’’ Aliongezea Kikwete.

Rais huyo wa zamani pia alisema kwamba alitajairia Magufuli angemaliza muhula wake na astaafu, ajiunge na familia yake lakini mipango ya Mungu ikawa tofauti.

Kulingana na Kikwete hakutarajia kwamba angemzika Magufuli lakini alijua angeishi maisha marefu ili awazike watangulizi wake.

Aidha, Kikwete alisema Mola alikuwa na sababu ya kumchukua akiwa bado mamlakani na ndio sababu amewapa Watanzania kiongozi mwingine mpya.

Rais Samia Suluhu amejaza Pengo la Rais Hayati Magufuli ambaye alingamizwa na maradhi ya moyo Machi, 17.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke