Wed, 26 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati amemfuta kazi Jaji Mkuu wa Mahakama ya Katiba, Danielle Darlan, na kumuwekea "kizuizi cha kudumu".
Agizo la Faustin Archange Touadera linakuja baada ya jaji huyo mwenye umri wa miaka 70 mwezi uliopita kutupilia mbali ombi la chama tawala la kufanyia marekebisho katiba ili aweze Rais Touadera kuwania muhula wa tatu.
Chama cha upinzani, Kwa Na Kwa, kilisema kimeshangazwa na amri hiyo, na kitaendelea kumtambua kama Mkuu wa Mahakama ya Katiba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live