Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru na na mtoto wa Museveni waonekana wakijituliza Nairobi

A6b247d0b8618a73 Rais Uhuru na na mtoto wa Museveni waonekana wakijituliza Nairobi

Fri, 1 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ingawa haikubainika ni eneo lipi haswa wawili hao walikuwa na ni kwa shughuli zipi, Muhoozi, alipakia picha kwenye Twitter akielekezea furaha yake kumtembelea Uhuru jijini Nairobi.

Mbali na ratiba zao zenye shughuli nyingi, wawili hao ambao walikuwa wamevalia mavazi ya kawaida, walionekana kufurahiya wakati wao pamoja.

Rais Uhuru Kenyatta na mwanwe Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni, Kamanda wa Vikosi vya Ardhi, Luteni Jenerali Muhoozi Kainerugaba, walionekana wakijituliza jijini Nairobi.

Ingawa haikubainika ni eneo lipi haswa wawili hao walikuwa na ni kwa shughuli zipi, Muhoozi, alipakia picha kwenye Twitter akielekezea furaha yake kumtembelea Uhuru jijini Nairobi.

Mbali na ratiba zao zenye shughuli nyingi, wawili hao ambao walikuwa wamevalia mavazi ya kawaida, walionekana kufurahiya wakati wao pamoja.

"Ni kwa heshima kuu nilijumuika na kakangu mkubwa na shujaa wangu hivi karibuni huko Nairobi. Rais Uhuru ni kielelezo kwa wengi wetu Afrika Mashariki na Afrika!" Kainerugaba aliandika.

Sio mara ya kwanza kwa Kainerugaba kuelezea kupendezwa kwake na Uhuru.

“Afande Uhuru Muigai Kenyatta. Rais wa Kenya na mtu mwenye heshima kubwa. Hamna yeyite anayeweza kuzuia reggae! Mungu ambariki,” Kainerugaba alisema katika chapisho mnamo Agosti 2021.

Vyombo vya habari vya Uganda viliripoti kuwa Kainerugaba alikuwa jijini Nairobi kufuatia ziara yake ya Somalia kati ya Septemba 23 na 27.

Wakati wa ziara yake, Luteni alimtembelea Rais wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmaajo, Waziri Mkuu Mohammed Hussein Roble na uongozi wa jeshi la AMISOM.

Alishirikiana pia na wanajeshi wa Uganda waliohusika katika operesheni dhidi ya Al Shabaab kwa nia ya kurejesha amani na utulivu nchini.

“Kusudi la ziara yangu ni kuwapongeza wanajeshi kwa kazi kubwa wanayoifanya nchini Somalia. Pili, ni kuzungumza nao na kujua changamoto wanazokabiliana nazo,” alisema.

Museveni ndiye Rais aliyehudumu kwa muda mrefu Afrika Mashariki na amekuwa akishinikiza shirikisho la majimbo ya Afrika Mashariki.

Yeye na Rais Uhuru wanafurahia ushirikiano na uhusiano mwema wa kibinafsi na kikazi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke