Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru azindua mfumo wa kidijitali katika Wizara ya Ardhi Kukomesha utapeli

03dfa2164045f7ef Rais Uhuru azindua mfumo wa kidijitali katika Wizara ya Ardhi Kukomesha utapeli

Wed, 28 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais Uhuru Kenyatta alisema jukwaa la kidijitali lilibuniwa ili kuimarisha usalama wa masuala ya ardhi na pia kuharakisha shughuli zinazofungamana na ardhi

- Uhuru alijuta kwamba Wakenya wengi wameanguka mikononi mwa matapeli na kupoteza mali zao

- Alisema kuwa kupitia jukwaa hilo, raia wataweza kupata habari zote za serikali juu ya ardhi

Rais Uhuru Kenyatta mnamo Jumanne, Aprili 27, alizindua mfumo wa kidijitali ili kukomesha masuala ya ulaghai unaoshuhudiwa katika idara ya ardhi kote nchini.

Jukwaa la usimamizi wa rasilimali ya ardhi lililopewa jina Ardhisasa lilibuniwa ili kuimarisha usalama wa ardhi na kurahisisha biashara inayofungamana na masuala ya ardhi.

Akiongea wakati wa uzinduzi, Uhuru alijuta kwamba wamekumbana na matapeli wanaposaka faili za mashamba yao ambazo mara kwa mara huwa wanahadaiwa zimepotea akisema kuwa kupitia mfumo huo wengi watapata afueni.

"Masuala ya faili za mashamba kutoweka ghafla, ufisadi na shughuli haramu za ardhi yatazikw akwenye kaburi la sahau," alisema.

Alisema kuwa Wakenya watasaidika mno na kwa urahisi kupitai mfumo huo ambapo pia itazuia mirundikano ya watu kwenye afisi za ardhi wakitafuta usaidizi.

Kiongozi wa taifa pia alisema kwamba mfumo huo ambao ulichukua miaka mitatu kabla ya kuwa tayari, ulibuniwa na vijana.

Rais alisisitiza kwamba watu wengine na wawekezaji pia watapata huduma za serikali na habari juu ya ardhi wakati wowote kwa haraka kwa njia iliyo wazi na salama wakati wowote.

"Mfumo huu wa kidijitali utawafikia wananchi kote nchini kwa awamu wakati tunapoendelea kujumuisha maoni ya wanaotumia.Tunakusudia kufika kila kona ya taifa 2022.

Jukwaa la Ardhisasa litasaidia pia kesi za mahakamani zinazochunguzwa na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa, Idara ya Upelelezi na vile vile DPP ili kuzuia udanganyifu katika sekta ya ardhi," Uhuru ameongeza.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke