Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru atoa zawadi ya mabasi 10 kwa shule, taasisi za kijamii

B78ca1f232fc4c20 Rais Uhuru atoa zawadi ya mabasi 10 kwa shule, taasisi za kijamii

Sat, 11 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta mnamo Ijumaa, Septemba 10, ametoa mabasi 10 kwa shule tofauti na taasisi mbali mbali za jamii nchini.

Rais alitoa mabasi hayo wakati wa sherehe iliyoandaliwa katika Ikulu, Nairobi

Hafla hiyo fupi ilikuwa ni kutambua uwepo wa Rais wa Estonia Kersti Kaljulaid ambaye yuko Kenya kwa ziara rasmi ya siku tatu

Mabasi hayo yalizawadiwa Shule ya Sekondari Tumutumu ya viziwi kaunti ya Nyeri, Shule ya Upili ya Marifano huko Tana River, Achego Girls Katika kaunti ya Kisumu na Shule ya sekondari Olorukuti katika kaunti ya Narok.

Mbali na shule hizo, Rais alitoa mabasi mengine kwa makundi ya kijamii, pamoja na Chama cha Wanawake Wakatoliki wa Dayosisi ya Maralal na kilabu cha Marafiki Football katika kaunti ya Nyeri.

Wengine waliofaidika na mpango huo ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Rukanga katika kaunti ya Kirinyaga, Shule ya Sekondari ya Mnagei huko Pokot Magharibi, AIC Moi Girls Maralal na Kisima Girls kutoka Kaunti ya Samburu.

Kaljulaid ndiye rais wa kwanza kutoka Estonia kuwahi kutembelea Kenya. Mbali na shughuli rasmi za kiserikali Rais Kaljulaid yuko Kenya kwa mazungumzo ya kujenga uhusiano mwema baina ya mataifa yote mawili.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi kadhaa wa kisiasa. Kiongozi wa wengi, Samuel Poghisio na Mbunge wa Kaunti ya Samburu Maison Leshomo walikuwa katika mkutanoni.

Wabunge kutoka Samburu Magharibi, Garsen, mji wa Nyeri, Kieni, Muhoroni, Mwea na Othaya pia walikuwepo.

Mbali na viongozi, hafla hiyo ilihudhuriwa na walimu na wanafunzi ambao walipokea zawadi ya mabasi.

Aidha kando na mabasi rais pia alitoa maski 2000 za kuoshwa kwa taasisi zilizokuwepo kwenye sherehe hiyo akilenga kusaida katika kudhibiti maambukizi ya COVID-19.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke