Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru alalamikiwa kuwa mbinafsi na kikwazo kwa wanasiasa

D27e6d6468c6721f Rais Uhuru alalamikiwa kuwa mbinafsi na kikwazo kwa wanasiasa

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria ameshutumu Rais Uhuru Kenyatta kwa kuwamaliza kisiasa viongozi wa maeneo ya Mlima Kenya.

Moses Kuria alisema eneo la Mt Kenya limekuwa kama madhabahu ya kutolea kafara, akitoa mfano wa waziri wa zamani wa kilimo aliyetimuliwa Mwangi Kiunjuri Kuria alidai kwamba Rais Uhuru Kenyatta amezima nyota za wanasiasa waliong'aa Mt Kenya, kama vile Paul Muite, Gitobu Imanyara na Martha Karua.

Mbunge huyo alidai kwamba, rais mstaafu Mwai Kibaki, ndiye rais wa pekee aliyewashika mkono viongozi wa Mt Kenya na kuwafanya kuwa bora

Kuria alidai kwamba Mt Kenya imekuwa ni kama madhabahu ya kutolea kafara taaluma ya siasa ya viongozi wa eneo hilo, akitoa mfano wa aliyekuwa waziri wa kilimo aliyefutwa kazi Mwangi Kiunjuri.

"Eneo hili limekuwa ni madhabahu ya kutoa kafara za taaluma ya kisiasa. Kwa mfano, miaka 25 iliyopita Mwangi Kiunjuri alichaguliwa kuwa mbunge na wenyeji wa Laikipia Mashariki. Robo karne baadaye, Kiunjuri aliyevuma anapanga kurudi Laikipia Mashariki ili awanie tena ubunge," Kuri alisema.

Kuria alishangazwa na hatua ya Uhuru ya kumfuta kazi mmoja kati ya mawaziri wawili wa kipekee wa Mt Kenya, kwa kipindi cha miaka kumi akiwa uongozini.

Mbunge huyo alisema sio Kiunjuri peke yake aliyemalizwa kisiasa, ila viongozi wengine kama vile; mbunge wa zamani Paul Muite na Gitobu Imanyara.

Alisema Martha Karua alikuwa aking'ang'ana, ila hana mshiko na ushawishi wa kisiasa kama alivyokuwa awali. Alisema haya yote yamesababishwa na Rais ambaye ndiye mfalme wa Mt. Kenya, aliyeshindwa kuwapa nafasi ya kukuza tajriba ya viongozi hao.

“Martha Karua anapata wakati mgumu kujaribu kuinua kichwa chake mbele ya umati mkubwa. Taaluma ya kisiasa ya Paul Muite ilinyauka kama mmea ambao hauwezi kuvunwa,” Kuria alisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke