Rais Uhuru Kenyatta ameondoka nchini na anasemekana yuko katika ziara rasmi ya kibiashara katika jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo kwa siku kadhaa
TUKO.co.ke imefahamishwa kwamba Uhuru alialikwa na Rais wa nchi hiyo na maraisa hao wawili wanatarajiwa kujadili maswala ya hapa na pale yanahusiana na biashara na maendeleo.
Uhuru aliandamana na viongozi kadhaa akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Raychelle Omamo, mwenzake wa Ugatuzi Eugene Wamalwa, Balozi wa Kenya mjini Kinshasha George Masafu na viongozi wengineo.
Ziara za Uhuru nchini Kongo inajiri siku moja baada ya Rais wa Somalia Mohammed Fatmajo pia kufanya mkutano wa kibiashara na rais wa nchi hiyo.