Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru Kenyatta aomboleza kifo cha Rais Mstaafu wa Zambia Kenneth Kaunda

B5efde180baab65b Rais Uhuru Kenyatta aomboleza kifo cha Rais Mstaafu wa Zambia Kenneth Kaunda

Fri, 18 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta ametuma risala za rambi rambi kwa mwenzake wa Zambia Edga Lungu kufuatia kifo cha rais mstaafu Kenneth KaundaKaunda ambaye alikuwa Rais wa kwanza wa Zambia, alifariki dunia Alhamisi, Juni 17 akiwa na umri wa miaka 17Uhuru alimtaja Kaunda kama kiongozi aliyepigania ukombozi wa Zambia na pia muungano wa mataifa ya Afrika Zambai inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Agosti 12, 2021 kumchagua rais mpya na wabungeRais Uhuru Kenyatta ameongoza Wakenya katika kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zambia Kenneth Kaunda.

Uhuru alituma rambi rambi zake kwa rais mwenzake wa Zambia Edgar Lungu, kwa serikali yake na wanachi kwa jumla.

Kaunda alifariki dunia Alhamisi, Juni 17 akiwa na umri wa miaka 97.

" Kwa niaba ya serikali na wananchi wa Kenya na kwa mimi binafsi, ningependa kutuma rambi rambi zangu kwa serikali ya Zambia na wananchi wake kufuatia kifo cha rais mstaafu Kenneth Kaunda," Uhuru aliomboleza.

Uhuru alimtaja Kaunda kama kiongozi aliye kuwa imara kupigania ukombozi wa nchi yake na muungano wa mataifa ya Afrika.

" Kaunda alikuwa kiongozi mwenye hekima ambaye aliendelea kujali masilahi ya mataifa mbali mbali ya Afrika licha ya kuondoka madakarani. Tutamkosa sana na tutamkumbuka kwa ustawi wake," Aliongezea Uhuru.

Uhuru aliongezea kwamba serikali yake itasimama na Zambia wakati huu mgumu wa majonzi na kuomba Mungu kwamba aendelee kuifariji.

Kifo cha Kaunda kilijiri siku tatu baada ya kulazwa katika hospitali ya jeshi ya Mwebantu mjini Lusaka. Hata hivyo familia yake haikutaja marehemu alikuwa akiigua ugonjwa upi.

"Tumempoteza rais wa kwanza wa Jamhuri ya Zambia Kenneth David Buchizya Kaunda kilichotokea mjini Lusaka baada ya kuugua kwa muda mfupi," Mwanawe Kaunda alisema. "

"Wengi watamkosa Bashikulu KK, Afrika nzima itamkumbuka, lala salama shujaa wetu Afrika," Aliongezea Kambarange.

Zambia inatarajia kufanya uchaguzi Agosti 12, 2021 kumchagua Rais mpya na wabunge.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke