Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru Kenyatta akata rufaa dhidi ya uamuzi wa BBI

193e5b603bd28bcf Rais Uhuru Kenyatta akata rufaa dhidi ya uamuzi wa BBI

Wed, 26 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Jopo la majaji watano lilisema BBI ambayo ilizaliwa kupitia handisheki kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa Upinzani Raila Odinga, ilichangiwa na rais mwenyewe kinyume cha sheria

- Mahakama kupitia uamuzi wake, ilihoji kuwa Rais Kenyatta alitumia vibaya mamlaka yake na kuenda kinyume cha sheria kukarabati Katiba

- Kiongozi wa taifa sasa anasema hakushirikishwa licha ya kuwa mshtakiwa katika kesi hiyo ya BBI

Rais Uhuru Kenyatta amewasilisha rufaa dhidi ya Mahakama Kuu kuhusu Mpango wa Maridhiano(BBI) ambao ulitaja mswada kuwa haramu, batili na tupu.

Kupitia wakili wake Waweru Gatonye, Uhuru alitoa sababu kadhaa za kutaka kukosoa uamuzi huo ambao ulimpata na makosa.

Hizi hapa sababu ambazo Uhuru alitoa:

1. Uhuru anataka kujua mbona anaweza kushtakiwa binafsi na wala si kama rais

2. Kiongozi wa taifa alisema hakushirikishwa licha ya kuwa mshtakiwa katika kesi hiyo ya BBI.

3. Uhuru hajaridhishwa na uamuzi kuwa alivunja sheria kukarabati Katiba ya 2010.

4. Amri mkuu wa majeshi anakosoa sababu kuwa anaweza kushtakiwa akiwa bado mamlakani endapo atakwenda kinyume cha sheria.

5. Uhuru anakosoa uamuzi kuwa anaweza tu kukarabati katiba kupitia mwanasheria mkuu na mpango wa bunge

6. Rais amesema kamati inayosimamia BBI haikuwa haramu kama ilivyodaiwa na jopo la majaji watano

Majaji Joel Ngugi, George Odunga, Jairus Ngaah, Chacha Mwita na Teresia Matheka walisema BBI ambayo ilizaliwa kupitia handisheki kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa Upinzani Raila Odinga, ilichangiwa na rais mwenyewe kinyume cha sheria.

Mahakama kupitia uamuzi wake, ilihoji kuwa Rais Kenyatta alitumia vibaya mamlaka yake na kuenda kinyume cha sheria kukarabati Katiba.

Pia ilizima lengo la BBI la kuunganisha taifa, ikisema itatimiza ajenda tofauti kwani mswada huo ulikuwa unapigiwa debe na Uhuru binafsi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke