Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru Afungua Roho, Asema Anajutia Kuingia Siasa

70d1b7a2e1bb008f Rais Uhuru Afungua Roho, Asema Anajutia Kuingia Siasa

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Video ya Rais akisema siasa ni kitu kisicho na maana katika maisha yake imesambaa mtandaoni

- Alisema alikuwa na wakati mzuri na marafiki kabla ya kuinhgia kwenye siasa na kutoa dhana kuwa kwa sasa anahangaika

- Wakenya wamekuwa wakimlima Rais kutokana na hatua ya serikali yake kuchukua mikopo nje

- Wanaharakati walianzisha kampeni mtandaoni ya kuirai benki ya fedha duniani kutoikopesha Kenya fedha zaidi

Rais Uhuru Kenyatta amefungua roho na kueleza kuwa anajutia kuingia kwenye ulingo wa siasa kwani hauna maana kwake.

Katika kile kimejitokeza kama kuelezea magumu anayopitia kwenye siasa, Rais alitaja ulingo wa siasa kama usio na maana yoyote kwake, 'useless'.

Kwenye video iliyosambaa mtandaoni, Rais Uhuru anamkumbuka mmoja wa waliokuwa marafiki wake kabla ya kuingia kwenye siasa.

"Tulikuwa na muda wa likizo pamoja kabla niingie kwenye ulingo huu wa siasa ambao hauna maana," alisema Rais na kuwaacha waliokuwepo kwa kicheko.

Ni video ambayo ilizua hisia mseto kutoka kwa Wakenya mtandaoni huku baadhi yao wakisema amefeli kwenye wajibu wake kama Rais na ndipo anatoa mazungumzo kama hayo.

Tatizo kubwa kwa wakosoaji wa Kenyatta ni kuhusiana na uamuzi wake wa kuomba mikopo ambayo wanasema itaishia kuwa mzigo mkubwa kwa walipa ushuru.

Baadhi ya wanaharakati walianzisha kampeni ya kuirai benki ya kimataifa IMF kutotoa mikopo zaidi kwa Kenya.

Rais Uhuru alichukua mkondo mpya wa siasa baada ya kuingia Ikulu kwa kipindi cha pili ambapo alifanya mkataba wa maelewano na kinara wa upinzani Raila Odinga.

Mkataba huo wa handisheki umemuweka katika njia panda kwani waliokuwa wandani wake wa kisiasa sasa wamegeuka na kuwa mahasimu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke