Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru Aagiza Baraza Lake la Mawaziri Kupokea Chanjo ya Covid-19 Mara Moja

547051498f3e203c Rais Uhuru Aagiza Baraza Lake la Mawaziri Kupokea Chanjo ya Covid-19 Mara Moja

Fri, 26 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais alisema mawaziri na wafanyakazi katika afisi ya Rais waongoze katika kupewa chanjo ya Covid-19

- Wakenya wamekuwa wakihofia chanjo hiyo na wengi kusema hawatapokea licha ya serikali kusema ina umuhimu mkubwa

- Wizara ya Afya ilisema wote waliofika umri wa miaka 58 kuenda juu wapewe kipau mbele

Rais Uhuru Kenyatta ameagiza baraza lake la mawaziri kupokea chanjo ya Covid-19 mara moja huku serikali ikipambana kukabili maambukizi ya coronavirus.

Tangazo hilo lilitolewa na mkuu wa wafanyikazi katika Ikulu Nzioka Waita Ijumaa Machi 26 wakati alipokea chanjo hiyo.

"Rais Uhuru ameagiza baraza lake la mawaziri na wafanyikazi wa afisi yake kutoa mfano bora na kupokea chanjo hiyo. Mimi nimepokea yangu asubuhi ya leo," alisema Waita.

Awali, Wizara ya Afya ilikuwa imetangaza kuwa itawapa kipau mbele wahudumu wa afya kupatiwa chanjo hiyo.

Hata hivyo sasa wizara imebadili hilo na kusema ongezeko la maambukizi ni hatari zaidi kwa waliotimia miaka 58 na zaidi na kwa hivyo watapewa kipau mbele.

Wakenya wamekuwa wakihofia uslaama wa chanjo hiyo jambo ambalo limefanya wengi kukosa kuchanjwa.

Naibu Rais William Ruto Alhamisi Machi 25 alisema yeye na Rais waliamua kutokuwa kwenye mstari wa mbele kuchanjwa kwa sababu hawako kwenye hatari kubwa.

"Tuliamua kusitisha mikutano ya hadhara kutokana na changamoto za corona…chanjo tulianza na wale watumishi ambao wako mstari wa mbele, haingekuwa mzuri kama mimi nimechanjwa na daktari ambaye yuko mstari wa mbele hana chanjo," alisema DP.

Aliwataka Wakenya kuhakikisha wanapokea chanjo hiyo ili kuweza kupigana na makali ya Covid-19.

“Ni vyema ya kwamba kila Mkenya unapopata nafasi ya kupata mchanjo…ni kizuizi kikubwa sana ya kupata maradhi haya yanayoletwa na corona.

Na mimi ikifika nafasi yangu, wakati itafika kiwango cha wale tunaofanya kazi hizi zingine, mimi ntakuwa mstari wa mbele pamoja na rais na mawaziri, kwa sababu tunataka kila Mkenya apate chanjo ndio tuweze kurudi katika hali ya kuendesha kazi zetu,” alisema DP.

Rais Uhuru anatarajiwa kuhutubia taifa Ijumaa Machi 26 kuhusu hali ya maradhi hayo wakati huu wimbi la tatu limeripotiwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke