Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Samia Suluhu amwacha Uhuru akivunja mbavu baada ya maneno matamu

06c0ecec020996ef Rais Samia Suluhu amwacha Uhuru akivunja mbavu baada ya maneno matamu

Wed, 5 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Suluhu alifika Kenya na ulimi mtamu huku maneno yake yakimyeyusha Rais Uhuru kila alipofika jukwaani kuzungumza

- Maneno kama 'Kaka Yangu' yalimtoka kwa upole uliokuwa umejaa utamu na kumfanya Rais kuhisi kweli ni ndugu wa Tanzania

- Jumatano Rais huyo wa sita Tanzania alicheza na maneno na kusema sasa kuna uhuru wa kufanya biashara na suluhu la vikwazo

Rais Samia Suluhu Jumatano Mei 5 aliwavunja mbavu wafanyibiashara wa Kenya na Tanzania alipowapa maneno matamu.

Rais Uhuru Kenyatta, ambaye pia alikuwepo, alionekana akifurahia kicheko kikali kutokana na ulimi wa Suluhu ulivyocheza na maneno.

Kwenye hotuba yake, Rais huyo wa sita Tanzania alisema serikali zote mbili zitahakikisha vikwazo vyote vya biashara vimeondolewa.

"Mna bahati kwamba katika nchi zetu mbili kwa upande mmoja kuna uhuru wa kufanya biashara na upande mwingine kuna suluhu za kuondosha vikwazo vya biashara," alisema na kuwaacha waliofika kikao hicho kwa kicheko.

Rais Kenyatta aliwataka wafanyibishara wa nchi hizi mbili kuhakikisha wananufaika na nafasi zinazoletwa na uhusiano bora.

Aliwataka wananchi wa Tanzania kuwekeza nchini Kenya akiahidi kuwa serikali yake itaondoa masharti ya kuwa na visa ya kufanya kazi pamoja na ya usafiri.

Kando na mtangulizi wake John Magufuli, Suluhu anaonekana kuchukua mkondo mpya kwenye uongozi haswa uhusiano wake na mataifa ya Afrika.

Kenya ndilo taifa la pili Suluhu kuzuru tangu achukue mamlaka ambapo alifanya ziara ya kwanza nchini Uganda kwa Yoweri Museveni.

Rais Uhuru alimwandalia makaribisho makubwa alipokagua guaride la heshima na kisha kuandaliwa sherehe ya usiku katika Ikulu.

Kabla ya kuondoka, Rais huyo atahutubia kikao cha bunge na seneti Jumatano alasiri kuelezea urafiki wa Kenya na Tanzania.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke