Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Samia Suluhu Kufanya Kikao na Yoweri Museveni Jumapili

7c5659bcb4826407 Rais Samia Suluhu Kufanya Kikao na Yoweri Museveni Jumapili

Sun, 11 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Samia atakuwa akifanya ziara yake ya kwanza nje ya Tanzania tangu kuchukua hatamu za uongozi

- Alichukua usukani mwezi Machi baada ya kifo cha aliyekuwa rais John Pombe

- Tanzania imeanza juhudi za kukarabati uhusiano wake na nchi za Afrika Mashariki

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Jumapili Aprili 11 atakuwa nchini Uganda kukutana na mwenzake Yoweri Kaguta Museveni.

Ziara hiyo nchini Uganda itakuwa ya kwanza kwa Rais Suluhu nje ya Tanzania tangu achukue hatamu za uongozi mwezi Machi baada ya kifo cha aliyekuwa mdosi wake John Pombe Magufuli.

Ripoti zimearifu kuwa Samia atapokelewa na Museveni baada ya kutua Uganda na kisha wawili hao waingie faraghani kwa mazungumzo.

Baadaye wawili hao watatia saini mkataba ambao utawezesha nchi hizo mbili kushirikiana katika mpango wa kupata mafuta.

Tanzania imekuwa ikiendeleza mikakati kuhakikisha uhusiano mwema kati yake na majirani katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kenya tayari imetuma kikosi cha kidiplomasia nchini Tanzania ambapo mazungumzo yaliandaliwa ili kujadili uhusiano kati ya mataifa hayo mawili.

Jumamosi Aprili 10, Waziri wa Michezo wa Kenya Amina Mohamed alikutana na Suluhu katika juhudi za kuleta Kenya na Tanzania pamoja.

Amina na Suluhu walifanya kikao katika Ikulu ambapo aliwasilisha ujumbe wa Rais Uhuru Kenyatta kwa rais huyo wa sita wa Tanzania.

Alimuomba kupanga ziara rasmi nchini Kenya katika kuendeleza urafiki kati ya mataifa hayo mawili.

Wakati wa uongzoi wa Magufuli, Tanzania na Kenya zilijipata na uhusiano baridi baada ya marais kuonekana kutofautiana.



Suala kuu lilikuwa kuhusu jinsi ya kupambana na janga la coronavirus ambapo Kenya iliweka masharti makali huku Tanzania ikisalia bila masharti yoyote.

Magufuli aliicheka Kenya kwa masharti yaliyoathiri uchumi huku Rais Kenyatta naye akisema 'majirani wetu walikuwa wameathirika pakubwa na janga hilo lakini wanaficha ukweli'.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama hapa kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke