Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Ruto ayakataa madeni utawala wake

Ruto Amsuta Raila Baada Ya Kutaka Seva Za IEBC Zifunguliwe Rais Ruto ayakataa madeni utawala wake

Wed, 12 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Kenya William Ruto amesema nchi hiyo haitakopa ili kuwalipa wafanyakazi wa umma hata kama vyama vya wafanyakazi vilitishia kugoma kutokana na kutolipwa mishahara ya Machi.

Ruto alilaumu ucheleweshaji wa deni kubwa la umma nchini, kutokana na baadhi ya mikopo kufikia hatua ya kulipwa mwezi huu.

Alisema mishahara hiyo italipwa kutokana na ushuru unaokusanywa na mamlaka ya mapato. Angalau mashirika mawili ya wafanyikazi yametoa notisi ya kugoma wiki hii ikiwa hawatalipwa pesa zao.

Akizungumza na vyombo vya habari siku ya Jumatatu, mshauri mkuu wa marais wa masuala ya kiuchumi alisema mishahara hiyo italipwa hadi mwisho wa mwezi lakini akashauri serikali kupunguza ufujaji wa fedha za umma.

Deni la umma la Kenya sasa linafikia asilimia sitini na tano ya mapato. Nchi inahitaji zaidi ya $420M kila mwezi kulipa mishahara na pensheni kwa watumishi wa umma.

Haya yanajiri wiki chache tu baada ya Benki ya Dunia na IMF kutoa onyo tofauti kwamba Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara inazama katika mgogoro mpya wa madeni, huku nchi nyingi zikiwa katika hatari kubwa ya kukumbwa na deni.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live