Thu, 30 May 2024
Chanzo: Bbc
Rais wa Kenya William Ruto amesema ndege yake aliyosafiri nayo kwenda Marekani iligharamiwa na walipa kodi wa Kenya kiasi cha chini ya milioni 10.
Ruto amesema kuwa baadhi ya marafiki wa Kenya ambão hakuwataja, walitoa ndege hiyo, baada ya kusema kuwa angesafiri na ndege ya shirika la Ndege la Kenya.
"Nilipoona mjadala Kenya kuhusu ni kwa namna gani nilisafiri kwenda Marekani na gharama mbalimbali zikielezwa kuwa….hii imegharimu milioni 200, hakuna namna ninayoweza kutumia sh milioni 200. Acha niwaambie hapa, hii imeigharimu kiasi cha chini ya shilingi milioni 10," alisema Rais Ruto.
Chanzo: Bbc