Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Ramaphosa akerwa na jambo hili

RAMAPHOSA ZA Rais Ramaphosa

Thu, 9 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Afrika Kusini amesema "amesikitishwa sana" na unyanyasaji wa raia wa kigeni wanaofanya kazi nchini humo.

Ni tatizo hasa katika kitongoji cha Alexandra, ambacho kilikuwa katikati ya ghasia za chuki dhidi ya wageni mwaka wa 2008. Baadhi ya wahamiaji huko wameiambia BBC kwamba sasa wanaishi kwa hofu.

"Walipokuja hapa kwa mara ya kwanza walikuwa saba. Walitulaza wote chini. Walichukua mashine, vifaa vya kukaushia nywele na mafuta. Hatukuwa na chaguo ila kuwaacha wazichukue kwa sababu walikuwa na bunduki".

David - si jina lake halisi ana ofisi ya kunyoa katika kitongoji cha Alexandra mjini Johannesburg.

David anasema washambuliaji wake walikuwa Waafrika Kusini, na kwamba kila wakati wanatoa masharti sawa kwamba anapaswa kuondoka nchini.

“Wanatuambia tunatakiwa kufunga biashara zetu, lakini sijui niende wapi,” anasema.

Pesa anazopata hapa zinasaidia familia yake huko Msumbiji. Lakini anasema yuko tayari kustahimili hatari yoyote inayokuja.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live