Rais Alassane Ouattara ametia saini amri ya kutoa Msamaha kwa mtangulizi wake, Laurent Gbagbo, aliyehukumiwa kifungo cha Miaka 20 jela mwaka 2018 kwa kukutwa na hatia ya kuhusika machafuko ya kisiasa nchini humo.
Rais Alassane Ouattara ametia saini amri ya kutoa Msamaha kwa mtangulizi wake, Laurent Gbagbo, aliyehukumiwa kifungo cha Miaka 20 jela mwaka 2018 kwa kukutwa na hatia ya kuhusika machafuko ya kisiasa nchini humo. Vile vile ametia saini amri ya kuachiliwa kwa masharti Washirika wa Gbagbo, akiwemo Mkuu wa zamani wa Jeshi la Wanamaji, Vagba Faussignaux na Kamanda wa Zamani wa kitengo muhimu cha kijeshi, Jean-Noel Abehi, waliotiwa hatiani kwa kuhusika katika machafuko ya baada ya uchaguzi wa Mwaka 2017.