Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo ameshinda muhula wa pili wa kiti hicho mara baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi nchini humo usiku wa kuhamkia leo, huku mpinzani wake John Mahama akipinga matokeo hayo na kusema atakwenda mahakamani.
Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Katika uchaguzi huo Akufo-Addo amepata asilimia 51.59 ya kura, akimpita kiongozi wa upinzani na Rais wa zamani wa taifa hilo Mahama aliyepata asilimia 47.36.
Licha ya nchi hiyo ya Afrika Magharibi kuwa inasifika kwa demokrasia thabiti, Mahama anapinga matokeo hayo kutokana na chama chake kushinda viti vingi vya ubunge na kusema kuwa zoezi zima la mchakato wa uchaguzi liligubikwa na udanganyifu mkubwa.