“Walinda usalama sasa wanatakiwa kutoa taarifa kwa umma ili kumaliza habari za kutekwa nyara ili watu wapate majibu ya kupotea kwa ndugu zao. Hilo ndilo suala kuu nilitaka kuzungumzia, kwani kumekuwa na habari kuu katika vyombo vya habari kuhusu kupotea kwa watu," amesema Rais Yoweri Kaguta Museveni
Museveni pia amevitaka vyombo vya usalama nchini Uganda kutoa taarifa za watu walio wakamta tangu wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana zifahamike ili familia zao zijue walipo na kuwafikia.
Tangazo hilo linadaiwa kutolewa na Rais Museveni baada ya familia nyingi nchini humo kulalamikia kupotea kwa wapendwa wao.