Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Mubarak kuzikwa leo

97153 Pic+mubarak Rais Mubarak kuzikwa leo

Wed, 26 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Cairo, Misri. Rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubaraka anatarajiwa kuzikwa leo.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la AFP, Rais huyo aliyefariki dunia jana akiwa na umri wa miaka 91 atazikwa kwa heshima za kijeshi.

Jumamosi iliyopita mtoto wa kiume wa kiongozi huyo, Alaa Mubarak aliandika katika ukurusa wake wa mtandao wa Twitter kuwa baba yake alikuwa akipatiwa matibabu katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Mtoto huyo alisema baba yake alifanyiwa upasuaji mwezi Januari lakini hakutoa ufafanuzi zaidi.

Viongozi mbali mbali wa dunia wametoa salamu zao za rambirambi wakisifu mchango wake alioutoa katika kusimamia nchi hiyo iliyopo Mashariki ya Kati.

Rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas alisema Mubarak alipigania haki za Wapalestina.

Pia Soma

Advertisement

 

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyau alisema  kiongozi huyo alihakikisha anasimamia amani na usalama wa watu wake na kukamilisha amani na Israel.

Ayman Nouur, mpinzani wa muda mrefu Misri na mgombea urais ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni nchini Uturuki alisema amemsamehe kiongozi huyo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz