Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Mstaafu Joseph Kabila atakiwa kurejesha jiwe la Almasi alilodhulumu

42432 Pic+kabila Rais Mstaafu Joseph Kabila atakiwa kurejesha jiwe la Almasi alilodhulumu

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirika la kiraia la NSCC nchini DRC limeendelea na kampeni yake ya kutaka Rais wa zamani wa nchi hiyo Joseph Kabila Kabange kurejesha almasi ambayo inadaiwa kuwa ni kubwa ambayo ni mali ya Théodore Ngoyi Kalala, kulingana na shirika hilo.

Hii ni kesi ambayo ilianza mwaka 2005 na ambayo pande hizo mbili tayari zilikubaliana suluhu ambayo Seneta Joseph Kabila bado hajaheshimu. Jiwe hilo lenye thamani kubwa linaaminika kuwa la mfanyabiashara Theodore Mbiya Kalala na awali liliibwa na wafanyabiashara wawili, kisha kulisafirisha hadi Antwerp, Ubelgiji, linasema shirika la NSCC.

Jumatatu hii NSCC imedai kurejeshwa kwa almasi hii yenye thamani ya dola bilioni 1. “Tunadai almasi ambayo Seneta Joseph Kabila alitunyang’anya. Almasi hii ni haki yetu. Almasi inanufaisha jimbo zima na si ya mtu mmoja pekee, Bw. Théodore Mbiye, bali ni ya watu wa Kasai ", amebaini Rachel Kapinga Ciamala, mratibu wa shirika la kiraia la NSCC katika mkoa wa Kasai Oriental.

Rufaa kwa Félix Tshisekedi

Barua hii tulioandika itatumwa kwa taasisi mbalimbali, “kudai marejesho au malipo ya thamani sawa na almasi hii. Bw. Joseph Kabila alikuwa tayari ameshajadiliana kuhusu bei ya almasi hii na mmiliki wake kwa dola za Marekani milioni 600 ”, shirika hilo limeongeza.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live