Thu, 12 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Malawi, Lazarus Chakwera, amewafukuza kazi waziri wa Nishati na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, kwa tuhuma za rushwa na ufisadi.
Wawili hao waliwalikamatwa Agosti 10,2021 kwa madai ya kuingilia utaratibu wa utoaji wa mikataba ya kusambaza mafuta.
Watuhumiwa hao pia walijaribu kushawishi jinsi ya kuratibu usambazaji wa mafuta kwa manufaa yao binafsi ili waweze kujitoea fedha hizo.
Mpaka sasa nafasi zao bado hazijajazwa,hivyo kupelekea Wizara hiyo kuwa chini ya ofisi ya rais hadi sasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live